BONYEZA LINK IFUATAYO KWA MAELEZO ZAIDI
ajira
Sunday, 27 August 2017
UMUHIMU WA KWENDA CHURCH
Kwa mtu MKITRO ni lazima kuhudhuria kanisani. Sio tu kwa sababu ni kitu kinachompendeza Mungu, bali pia ni kwa ajili ya kukua na kuimarika kiroho. Kuna sababu nyingi za kiMungu zinazotufanya tuhudhurie ibada kanisani, hapa kuna baadhi ya hizo
1. Ni udhihirisho wa upendo wetu kwa Mungu
Kuhudhuria ibada kanisani ni udhihirisho halisi na unaoonekana wa upendo wetu kwa Mungu. Ni mahali tunapoweza kumtolea Mungu dhabihu za sifa, shukrani na heshima.
Zaburi 134:2 Inueni mikono yenu katika mahali patakatifu
na mumsifu BWANA .
Tunapaswa kumtolea Mungu muda na nguvu zetu katika kumwabudu na kumsifu maana yeye pekee ndiye anayestahili.
Ufunuo 4:11 Bwana wetu na Mungu wetu, wewe umestahili kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa maana ni wewe uliyeviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako vitu vyote viliumbwa na vinapata kuwapo.”
2. Tunaimarika Kiroho
Tunaposikia neno la Mungu likihubiriwa na kufundishwa kanisani imani yetu inakua na roho zetu zinaimarika. Ni muhimu kwa roho zetu kuwa na akiba ya neno la Mungu la kutuwezesha kuvuka pale tunapokutana na changamoto mbali mbali. Ni muhimu kutumia kila nafasi tunayoipata kujivika silaha za Mungu ili tuweze kumshinda adui, na tunapohudhuria kanisani tunapata kulishwa neno la Mungu, kutiwa moyo na kuimarishwa roho zetu. Neno la Mungu ndilo linatuimarisha na kujenga imani yetu.
Warumi 10:17 Basi, chanzo cha imani ni kusikia, na kusikia huja kwa kuhubiri neno la Kristo.
3. Tunapata nafasi ya kuwa katika uwepo wa Mungu
Kuna ahadi ya Mungu kuwa wakutanapo wawili au watatu yeye anakuwa kati kati yao, watu wanaojihudhurisha pamoja kwa ajili ya kumtafuta. Pamoja na kwa Yesu yupo ndani yetu, anadhamini sana mkutaniko wa watu wanaokutanika kwa ajili ya kumuomba, kumsifu, kumuabudu na kumsikiliza. Mahali kama hapo Mungu anashusha uwepo wake, upako na nguvu zake.
Mathayo 18:20 Kwa maana wanapokutana watu wawili au watatu katika jina langu, hapo mimi nipo pamoja nao
Na katika uwepo hu wa Mungu, Roho Mtakatifu anashusha vipawa vyake na karama mbalimbali.
4. Inaleta umoja katika kanisa la Mungu
Tnapokutanika pamoja kwenye ibada tunapata kufahamiana na wapendwa wengine na kuleta umoja miongoni mwa watu tunaomwamini Mungu. Uhusiano mzuri na Mungu unahitaji pia kuwa na uhusiano mzuri na watu wa Mungu. Huwezi kumpenda Mungu na kumchukia ndugu yako.
1 Yohana 2:9-10 Mtu anayesema kwamba anaishi nuruni, naye anamchukia ndugu yake, bado yumo gizani. 10Anayempenda ndugu yake anaishi katika nuru na wala hana kitu cha kumfanya ajikwae
Huwezi kuwa na uhusianao na watu usiowajua wala kukutana nao hivyo kwenda kanisani kunakupa nafasi ya kukutana na kufahamiana na watu wa Mungu.
1 Yohana 1:7 Bali tukiishi nuruni, kama yeye alivyo nuru, tunakuwa na ushirika sisi kwa sisi na damu ya Mwanae Yesu, inatutakasa dhambi zote
5. Ni ishara ya utii kwa Mungu
Kwenda kanisani ni ishara ya kuonyesha utii kwa Mungu na kwa neno lake. Neno la Mungu linatuasa tusiache kukutanika pamoja.
Ebrania 10: 24-25 Na tujishughulishe kutafuta jinsi ya kuhimizana katika kuonyeshana upendo na kutenda mema. Tusiache kukutana pamoja, kama wengine wanavyofanya, bali tutiane moyo, hasa zaidi tunapoona siku ile ikikaribia.
Kukutanika huku kunatupa nafasi ya kuimarishana, kutiana mouo, kuinuana na kufarijiana na wapendwa wengine. Ukifahamu umuhimi wa kenda kanisani nawe ukawa hufanyi hivyo utakuwa unamkosea Mungu.
Yakobo 4:17 Mtu ye yote anayefahamu lililo jema kutenda, lakini asilitende, basi mtu huyo anatenda dhambi.
1. Ni udhihirisho wa upendo wetu kwa Mungu
Kuhudhuria ibada kanisani ni udhihirisho halisi na unaoonekana wa upendo wetu kwa Mungu. Ni mahali tunapoweza kumtolea Mungu dhabihu za sifa, shukrani na heshima.
Zaburi 134:2 Inueni mikono yenu katika mahali patakatifu
na mumsifu BWANA .
Tunapaswa kumtolea Mungu muda na nguvu zetu katika kumwabudu na kumsifu maana yeye pekee ndiye anayestahili.
Ufunuo 4:11 Bwana wetu na Mungu wetu, wewe umestahili kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa maana ni wewe uliyeviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako vitu vyote viliumbwa na vinapata kuwapo.”
2. Tunaimarika Kiroho
Tunaposikia neno la Mungu likihubiriwa na kufundishwa kanisani imani yetu inakua na roho zetu zinaimarika. Ni muhimu kwa roho zetu kuwa na akiba ya neno la Mungu la kutuwezesha kuvuka pale tunapokutana na changamoto mbali mbali. Ni muhimu kutumia kila nafasi tunayoipata kujivika silaha za Mungu ili tuweze kumshinda adui, na tunapohudhuria kanisani tunapata kulishwa neno la Mungu, kutiwa moyo na kuimarishwa roho zetu. Neno la Mungu ndilo linatuimarisha na kujenga imani yetu.
Warumi 10:17 Basi, chanzo cha imani ni kusikia, na kusikia huja kwa kuhubiri neno la Kristo.
3. Tunapata nafasi ya kuwa katika uwepo wa Mungu
Kuna ahadi ya Mungu kuwa wakutanapo wawili au watatu yeye anakuwa kati kati yao, watu wanaojihudhurisha pamoja kwa ajili ya kumtafuta. Pamoja na kwa Yesu yupo ndani yetu, anadhamini sana mkutaniko wa watu wanaokutanika kwa ajili ya kumuomba, kumsifu, kumuabudu na kumsikiliza. Mahali kama hapo Mungu anashusha uwepo wake, upako na nguvu zake.
Mathayo 18:20 Kwa maana wanapokutana watu wawili au watatu katika jina langu, hapo mimi nipo pamoja nao
Na katika uwepo hu wa Mungu, Roho Mtakatifu anashusha vipawa vyake na karama mbalimbali.
4. Inaleta umoja katika kanisa la Mungu
Tnapokutanika pamoja kwenye ibada tunapata kufahamiana na wapendwa wengine na kuleta umoja miongoni mwa watu tunaomwamini Mungu. Uhusiano mzuri na Mungu unahitaji pia kuwa na uhusiano mzuri na watu wa Mungu. Huwezi kumpenda Mungu na kumchukia ndugu yako.
1 Yohana 2:9-10 Mtu anayesema kwamba anaishi nuruni, naye anamchukia ndugu yake, bado yumo gizani. 10Anayempenda ndugu yake anaishi katika nuru na wala hana kitu cha kumfanya ajikwae
Huwezi kuwa na uhusianao na watu usiowajua wala kukutana nao hivyo kwenda kanisani kunakupa nafasi ya kukutana na kufahamiana na watu wa Mungu.
1 Yohana 1:7 Bali tukiishi nuruni, kama yeye alivyo nuru, tunakuwa na ushirika sisi kwa sisi na damu ya Mwanae Yesu, inatutakasa dhambi zote
5. Ni ishara ya utii kwa Mungu
Kwenda kanisani ni ishara ya kuonyesha utii kwa Mungu na kwa neno lake. Neno la Mungu linatuasa tusiache kukutanika pamoja.
Ebrania 10: 24-25 Na tujishughulishe kutafuta jinsi ya kuhimizana katika kuonyeshana upendo na kutenda mema. Tusiache kukutana pamoja, kama wengine wanavyofanya, bali tutiane moyo, hasa zaidi tunapoona siku ile ikikaribia.
Kukutanika huku kunatupa nafasi ya kuimarishana, kutiana mouo, kuinuana na kufarijiana na wapendwa wengine. Ukifahamu umuhimi wa kenda kanisani nawe ukawa hufanyi hivyo utakuwa unamkosea Mungu.
Yakobo 4:17 Mtu ye yote anayefahamu lililo jema kutenda, lakini asilitende, basi mtu huyo anatenda dhambi.
MUNGU akubariki ana.
Neema za Kristo.
Saturday, 26 August 2017
Wednesday, 11 January 2017
MFAHAMU HERODE
Leo nimeonelea tujifunze juu ya habari ya Herode mfalme.
Karibu…
*Kwanza kabisa napenda ufahamu kuwa jina la Herode ni jina la Wafalme linalowakilisha Wafalme wanne waliotawala kati ya sehemu ndogo
au sehemu yote katika ya Yuda (Judea) chini ya utawala wa WARUMI na wanaelezewa vizuri katika agano jipya.
Sasa tuanze kumuangalia HERODE wa kwanza;
01 HERODE MKUU(. HEROD THE GREAT,)
*Huyu alikuwa ni mtoto wa Antipater ambaye alikuwa na kibali kikubwa kwa Juliasi Sizelia (Julius Caesar.)
Katika umri wake wa miaka kumi na mitano,HERODE alikabidhiwa kikatiba na baba yake aitawale GALILAYA chini ya Hyrcanus II,
ambaye alikuwa ni kiongozi wa Taifa la WAYAUDI.
Madaraka ya Hyrcanus yalikuwa yakipingwa na kaka yake Aristobulus.
*Habari za Herode mkuu zimeelezwa pia katika Mathayo 2:1-23,na Luka ,1:5.
Hata hivyo Herode alihofia utawala huo na kuamua kwenda RUMI na huko ndiko akajulikana kama mfalme wa YUDA , ( B. C. 37. )
*Na ikumbukwe kuwa huyu Herode ndie Yule aliyeamuru mauaji ya watoto wote wenye umri wa miaka miwili,ili aweze kumuangamiza Yesu huko Betrehemu ya Uyahudi.
*Mara tu baada ya kifo cha Herode ,Nusu ya ufalme wake ,ikijumuisha Yuda, Ideumaea, na Samalia,ulitwaliwa na mtoto wake Archelaus,mbapo ufalme wake uliobakia uligawanywa katikati ya watoto wake wengine wawili Herod Antipas na Philip.
2. HEROD PHILIP.
*Huyu alikuwa ni mtoto wa Herode mkuu,naye hujulikana kama HERODE lakini ili kuwatofautisha yeye na baba yake ni lazima umuite baba yake kuwa ni Herode mkuu,na huyu umuite Herode Philip
3. HEROD ANTIPAS,
Huyu Herode wa tatu alikuwa pia ni mtoto wa Herode mkuu,ambaye alitoka kwa mwanamke Malthace ,
Msamaria.Soma Luka 3:1,
*Antipas alipata elimu yake huko Rumi.Baada ya kufa baba yake (Herode mkuu) aliteuliwa na kuiangalia Galilaya na Perea ,sehemu ya kusini mwa nchi na ni mashariki mwa Yordani.
*Herode Antipas ndiye Yule Herode aliyepelekea kifo cha Yohana mbatizaji kwa kukatwa kichwa chake akiwa gerezani. Soma Mathayo 14 :1-12,
Pia Herode Antipas anaonekana kuwa ni mfuasi wa Masadukayo Mathayo 16:6 .
4.(i) HERODE AGRIPPA MKUU.(Au Agrippa wa kwanza)
Huyu alikuwa ni mjukuu wa Herode mkuu,(Herod the great)
Waweza kusoma habari zake pia katika Matendo 12: :1-25,
Na ndie aliyemua Yakobo ndugu yake YOHANA
Tunasoma Matendo 12 :1-21
“ Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa.
Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga.”
*Agrippa mkuu alikuwa ni mtu aliyeshika YUDA na Samaria ambazo babu yake alikuwa ndio muanzilishi A.D.43
(ii). HERODE AGRIPPA MDOGO (au Herode Agrippa wa pili)
*Huyu ni mtoto wa Agrippa wa kwanza,(Herode Arippa mkuu)Naye alipata elimu yake huko Rumi chini ya usimamizi wa Claudio ( Claudius.)
*Pia habari zake zinaonekana katika Matendo 25 :1-26,Tena katika mstari wa 13 Linalomeka hivi hilo andiko ;
“ Siku kadha wa kadha zilipokwisha kupita,AGRIPA MFALME na Bernike wakafika Kaisaria, wakimwamkia Festo.”
Katika kifo cha baba yake ambapo alikuwa na umri wa miaka kumi na saba (17).
Alikufa akiwa na umri wa miaka sabini katika mwaka wa tatu wa Trajan (Trajan's reign,) Bwana Yesu asifiwe…
Tunasoma Matendo 12 :1-21
“ Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa.
Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga.”
*Agrippa mkuu alikuwa ni mtu aliyeshika YUDA na Samaria ambazo babu yake alikuwa ndio muanzilishi A.D.43
(ii). HERODE AGRIPPA MDOGO (au Herode Agrippa wa pili)
*Huyu ni mtoto wa Agrippa wa kwanza,(Herode Arippa mkuu)Naye alipata elimu yake huko Rumi chini ya usimamizi wa Claudio ( Claudius.)
*Pia habari zake zinaonekana katika Matendo 25 :1-26,Tena katika mstari wa 13 Linalomeka hivi hilo andiko ;
“ Siku kadha wa kadha zilipokwisha kupita,AGRIPA MFALME na Bernike wakafika Kaisaria, wakimwamkia Festo.”
Katika kifo cha baba yake ambapo alikuwa na umri wa miaka kumi na saba (17).
Alikufa akiwa na umri wa miaka sabini katika mwaka wa tatu wa Trajan (Trajan's reign,)
*Kwanza kabisa napenda ufahamu kuwa jina la Herode ni jina la Wafalme linalowakilisha Wafalme wanne waliotawala kati ya sehemu ndogo
au sehemu yote katika ya Yuda (Judea) chini ya utawala wa WARUMI na wanaelezewa vizuri katika agano jipya.
Sasa tuanze kumuangalia HERODE wa kwanza;
01 HERODE MKUU(. HEROD THE GREAT,)
*Huyu alikuwa ni mtoto wa Antipater ambaye alikuwa na kibali kikubwa kwa Juliasi Sizelia (Julius Caesar.)
Katika umri wake wa miaka kumi na mitano,HERODE alikabidhiwa kikatiba na baba yake aitawale GALILAYA chini ya Hyrcanus II,
ambaye alikuwa ni kiongozi wa Taifa la WAYAUDI.
Madaraka ya Hyrcanus yalikuwa yakipingwa na kaka yake Aristobulus.
*Habari za Herode mkuu zimeelezwa pia katika Mathayo 2:1-23,na Luka ,1:5.
Hata hivyo Herode alihofia utawala huo na kuamua kwenda RUMI na huko ndiko akajulikana kama mfalme wa YUDA , ( B. C. 37. )
*Na ikumbukwe kuwa huyu Herode ndie Yule aliyeamuru mauaji ya watoto wote wenye umri wa miaka miwili,ili aweze kumuangamiza Yesu huko Betrehemu ya Uyahudi.
*Mara tu baada ya kifo cha Herode ,Nusu ya ufalme wake ,ikijumuisha Yuda, Ideumaea, na Samalia,ulitwaliwa na mtoto wake Archelaus,mbapo ufalme wake uliobakia uligawanywa katikati ya watoto wake wengine wawili Herod Antipas na Philip.
2. HEROD PHILIP.
*Huyu alikuwa ni mtoto wa Herode mkuu,naye hujulikana kama HERODE lakini ili kuwatofautisha yeye na baba yake ni lazima umuite baba yake kuwa ni Herode mkuu,na huyu umuite Herode Philip
3. HEROD ANTIPAS,
Huyu Herode wa tatu alikuwa pia ni mtoto wa Herode mkuu,ambaye alitoka kwa mwanamke Malthace ,
Msamaria.Soma Luka 3:1,
*Antipas alipata elimu yake huko Rumi.Baada ya kufa baba yake (Herode mkuu) aliteuliwa na kuiangalia Galilaya na Perea ,sehemu ya kusini mwa nchi na ni mashariki mwa Yordani.
*Herode Antipas ndiye Yule Herode aliyepelekea kifo cha Yohana mbatizaji kwa kukatwa kichwa chake akiwa gerezani. Soma Mathayo 14 :1-12,
Pia Herode Antipas anaonekana kuwa ni mfuasi wa Masadukayo Mathayo 16:6 .
4.(i) HERODE AGRIPPA MKUU.(Au Agrippa wa kwanza)
Huyu alikuwa ni mjukuu wa Herode mkuu,(Herod the great)
Waweza kusoma habari zake pia katika Matendo 12: :1-25,
Na ndie aliyemua Yakobo ndugu yake YOHANA
Tunasoma Matendo 12 :1-21
“ Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa.
Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga.”
*Agrippa mkuu alikuwa ni mtu aliyeshika YUDA na Samaria ambazo babu yake alikuwa ndio muanzilishi A.D.43
(ii). HERODE AGRIPPA MDOGO (au Herode Agrippa wa pili)
*Huyu ni mtoto wa Agrippa wa kwanza,(Herode Arippa mkuu)Naye alipata elimu yake huko Rumi chini ya usimamizi wa Claudio ( Claudius.)
*Pia habari zake zinaonekana katika Matendo 25 :1-26,Tena katika mstari wa 13 Linalomeka hivi hilo andiko ;
“ Siku kadha wa kadha zilipokwisha kupita,AGRIPA MFALME na Bernike wakafika Kaisaria, wakimwamkia Festo.”
Katika kifo cha baba yake ambapo alikuwa na umri wa miaka kumi na saba (17).
Alikufa akiwa na umri wa miaka sabini katika mwaka wa tatu wa Trajan (Trajan's reign,) Bwana Yesu asifiwe…
Tunasoma Matendo 12 :1-21
“ Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa.
Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga.”
*Agrippa mkuu alikuwa ni mtu aliyeshika YUDA na Samaria ambazo babu yake alikuwa ndio muanzilishi A.D.43
(ii). HERODE AGRIPPA MDOGO (au Herode Agrippa wa pili)
*Huyu ni mtoto wa Agrippa wa kwanza,(Herode Arippa mkuu)Naye alipata elimu yake huko Rumi chini ya usimamizi wa Claudio ( Claudius.)
*Pia habari zake zinaonekana katika Matendo 25 :1-26,Tena katika mstari wa 13 Linalomeka hivi hilo andiko ;
“ Siku kadha wa kadha zilipokwisha kupita,AGRIPA MFALME na Bernike wakafika Kaisaria, wakimwamkia Festo.”
Katika kifo cha baba yake ambapo alikuwa na umri wa miaka kumi na saba (17).
Alikufa akiwa na umri wa miaka sabini katika mwaka wa tatu wa Trajan (Trajan's reign,)
Subscribe to:
Comments (Atom)
